Home KITAIFA DC MTATIRO ATANGAZA KUWAFUKUZA WAFUGAJI WASIOTAKA KWENDA KWENYE VITALU

DC MTATIRO ATANGAZA KUWAFUKUZA WAFUGAJI WASIOTAKA KWENDA KWENYE VITALU

Google search engine
Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Wakili Julius Mtatiro akikata utepe kufungua ikiwa ni ufunguzi rasmi wa nyumba ya kulala wageni  ya Kajima Guest House iliyojengwa na mfugaji Mahimbo Shamba.

Na Muhidin Amri,Tunduru

SERIKALI ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma, imesema itawakamata na kuwatoza faini  kubwa wafugaji  wote wanaoishi kiholela na kuchunga mifugo nje ya maeneo yaliyotengwa (vitalu).

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa wilaya hiyo, Julius Mtatiro wakati akizungumza na wafugaji wakati wa ufunguzi wa nyumba ya kulala wageni ya Kajima Guest House iliyojengwa na mfugaji wa jamii ya Kisukuma Mahembo Shamba.

Mfugaji huyo amelazimika kuuza sehemu ya mifugo yake na kujenga nyumba ya kulala wageni, ikiwa ni utekelezaji wa agiza la serikali linalowataka wafugaji kupunguza mifugo na kuwekeza kwenye miradi mingine ya maendeleo.

Kwa mujibu wa Mtatiro, licha ya mapenzi makubwa ya serikali kwa jamii ya wafugaji wilayani humo, lakini bado kuna  wafugaji  wanakahidi na kufanya ufugaji kiujanja ujanja kwenye makazi ya wakulima na kusababisha migogoro mingi kati ya makundi  hayo mawili.

Amesema, Wilaya ya Tunduru ni ya kilimo licha ya kukaribisha wafugaji, hata hivyo suruhisho la migogoro inayojitokeza kati ya wakulima na wafugaji ni lazima wafugaji wakapelekwa katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli zao.

Mtatiro, amempongeza mfugaji huyo kwa kuitikia wito wa serikali kwa kupunguza idadi ya mifugo yake na kufanya uwekezaji wa nyumba ya wageni na kuwataka wafugaji wengine kuiga mfano huo.

Kwa upande wake mfugaji huyo amesema,amelazimika kujenga nyumba ya wageni baada ya kupoteza sehemu kubwa ya mifugo yake mkoani Mbeya na Morogoro na amelazimika kuja wilayani Tunduru baada ya kusikia kuna mazingira mazuri  kwa ajili ya kuchungia.

Amesema, hadi kukamilika kwa nyumba hiyo  yenye vyumba 10 vya kulala wageni ametumia fedha nyingi baada ya kuuza ng’ombe 220 na kuwataka wafugaji wengine kupunguza mifugo yao na kuwekeza katika miradi mingine ya kiuchumi.

Baadhi ya wananchi wa jamii ya kifugaji waliohudhuria ufunguzi wa nyumba ya kulala wageni ya Kajimba Guest House inayomilikiwa na mfugaji Mahimbo Shamba.
Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here