Home KITAIFA Tanzania, Voice of Nigeria wafungua darasa la Kiswahili kwa wafanyakazi wake

Tanzania, Voice of Nigeria wafungua darasa la Kiswahili kwa wafanyakazi wake

Google search engine
Balozi wa Tanzania nchini, Nigeria, Dk. Benson Banna, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Idhaa ya Voice of Nigeria

Na Mwandishi Maalumu

-NIGERIA

UBALOZI wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Voice of Nigeria, umefungua Darasa la Kiswahili kwa wafanyakazi wa Voice of Nigeria.

Mafunzo hayo ni kwa ngazi ya awali kwa ajili VON kujiandaa kuimarisha Idhaa yao ya Kiswahili, yalifanyika Mei 9, 2023

Mafunzo yalifunguliwa na Balozi Benson Alfred Bana, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Nigeria na Mkurugenzi wa VON, Osita Okechukwu

Aidha, VON September 23, 2022 walisaini hati ya makubaliano na TBC, ambapo pamoja na mambo mengine kwa ajili ya kushirikiana katika Kutangaza Kiswahili.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here