Home KITAIFA DK. MWINYI-SERIKALI IMEFANIKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI

DK. MWINYI-SERIKALI IMEFANIKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI

Google search engine
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi

Na MWANDISHI WETU

-ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imefanikiwa sana kuongeza ukaribu  na wananchi kwa kusikiliza changamoto na kuzitatua kwa haraka kupitia Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi (SNR).

Rais Dk.Mwinyi amesema  Mfumo wa SNR  ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wananchi pia ni kigezo cha utawala bora unaozingatia ushirikishwaji wa wananchi.

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo katika hafla ya Maadhimisho ya miaka mitatu ya Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi(SNR) tarehe: 16 Machi 2024 katika Viwanja vya Ikulu Mnazi Mmoja.

Aidha, Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa  kitengo cha SNR kina wajibu kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kutumia njia mbalimbali kwa wananchi ili waweze kutumia vema Mfumo huu kwa madhumuni yaliyokusudiwa.

Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi amesema katika kipindi cha Miaka 3 tangu kuanzishwa kwa Mfumo wa SNR jumla la malalamiko 13,517 yamepokelewa  kati ya hayo 11,116 yamepatiwa ufumbuzi na 2,351 yanaendelea kufanyiwa kazi katika hatua mbalimbali.

Viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyombo vya ulinzi na usalama na Vyama vya Siasa wamehudhuria hafla hiyo.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here