Home KITAIFA DPP AMFUTIA KESI DK. PIMA, AMFUNGULIA KESI MPYA MBILI

DPP AMFUTIA KESI DK. PIMA, AMFUNGULIA KESI MPYA MBILI

Google search engine

Na MWANDISHI WETU

-ARUSHA

MKURUGENZI wa Mashtaka nchini DPP amemfutia kesi na kumfungulia mpya mbili za uhujumu uchumi aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Dk. John Pima na wenzake watatu.

Kesi hizo zimefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, zikimkabili na wenzake watatu.

Kesi hizo zina mashtaka nane kila moja ikiwemo ya ufujaji na ubadhirifu wa milioni 65 fedha za Serikali.

Katika maelezo ya kesi inadaiwa walijipatia kiasi hicho kwa kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri kuwa wamezitumia fedha hizo kumwaga Moramu katika Masoko ya Kilombero, Soko Kuu, Mbauda na Morombo jambo ambalo sio kweli.

Washtakiwa wote wamekana mashtaka huku watatu wakiachiwa kwa dhamana.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here