Home KITAIFA MEYA KINONDONI AIPONGEZA PLAN INTERNATIONAL KUTOA MSAADA KWA WASIOONA

MEYA KINONDONI AIPONGEZA PLAN INTERNATIONAL KUTOA MSAADA KWA WASIOONA

Google search engine
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Uchechemuzi Shirika la Plan International  Cecilia Bosco (kulia) akimkabidhi Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Songoro Mnyonge baadhi ya vifaa saidizi ambavyo vimegawiwa kwa Jumuiya ya Wasioona Tanzania ( TAB). Hafla hiyo imefanyika Jijini Dar es Salaam.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Songoro Mnyonge akizungumza katika hafla ya magabidhiano ya msaada wa vifaa saidizi kwa Jumuiya ya watu wasioona Tanzania, ambavyo vimetolewa na Shirika la Plan International

Na MWANDISHI WETU

-DAR ES SALAAM

MEYA wa Halmashauri y Manispaa ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Songoro Mnyonge amelipongeza Shirika la Plan International kwa kutoa msaada wa vifaa saidizi kwa Jumuiya ya Wasioona Tanzania ( TAB) vyenye thamani ya zaidi ya Silingi milioni tisa.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo Machi 21,2024 katika Ofisi za (TAB) Jijini Dar es Salaam, Mnyonge amesema wasioona wanapitia wakati mgumu pindi wanapokosa vifaa saidizi ambavyo vingeweza kuwasaidia kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.

“Nimesikia kuna wengine wametokea Buza, Kigamboni, Goba na maeneo mengine ya mbali na kufika hapa ofisini kwao, wamekuwa wakipatiwa msaada na wananchi wa maeneo ya Kinondoni kufika kwenye neoe hili la ofisi, hivyo basi kuna umuhimu wakapata vifaa saidizi,” amesema Meya Mnyonge.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Uchechemuzi Shirika la Plan International, Cecilia Bosco amesema vifaa hivyo vitawasaidia kutoka kwenda katika Shughuli zao za kila siku za kujipatia kipato.

Kutokana na na hali hiyo, amesema wameipatia taasisi ya watu wasioona vifaa ambavyo ni fimbo nyeupe 100, Karatasi za kijivu pisi 100 pamoja na A4 fremu pisi 50 ambazo hutumika wanapokuwa wanaandika ambapo itawasaidia katika shughuli zao.

Amesema wataendelea kuimarisha nakuongeza nguvu kuwasaidia watu wasioona pamoja na makundi mbalimbali yenye mahitaji maalumu nchini kwa lengo la kupunguza changamoto wanazozipitia.

Wanachama wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania ( TAB) wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Songoro Mnyonge pamoja na wawakilishi kutoka Shirika la Plan International mara baada ya Shirika hilo kukabidhi msaada wa vifaa saidizi kwa TABWanachama wa Jumuiya ya Wasioona Tanzania ( TAB) wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mhe. Songoro Mnyonge pamoja na wawakilishi kutoka Shirika la Plan International mara baada ya Shirika hilo kukabidhi msaada wa vifaa saidizi kwa TAB

Naye Mtunza hazina wa Jumuiya ya Watu Wasioona Tanzania, Seif Hamis amesema vifaa hivyo ni muhimu ambapo itawasaidia kuzifikia fursa mbalimbali.

Aidha ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambapo imefungua  milango ya fursa mbalimbali ikiwamo kwa watu wasioona.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here