Home KITAIFA BALOZI DK. NCHIMBI ANA KWA ANA NA DK. SHEIN, SALMIN AMOUR ‘KOMANDOO’...

BALOZI DK. NCHIMBI ANA KWA ANA NA DK. SHEIN, SALMIN AMOUR ‘KOMANDOO’ VISIWANI ZANZIBAR

Google search engine
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, akizungumza na Rais Mstaafu na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Salmin Amour, leo Machi 25, 2024 Jijini Zanzibar
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, akizungumza na Rais Mstaafu na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, leo Machi 25, 2024 Jijini Zanzibar

Na MWANDISHI MAALUM

-ZANZIBAR

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, amesema ushauri na maelekezo ya viongozi wastaafu wa Chama na Serikali, pamoja na wazee wa CCM kuhusu umuhimu wa kuendelea kukiimarisha Chama, ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwatumikia watu vizuri, yatafanyiwa kazi kwa uzito unaostahili.

Katibu Mkuu Balozi Dk. Nchimbi amesema hayo Jumapili, Machi 24, 2024, wakati wa mazungumzo na viongozi wastaafu wa Chama na Serikali, wakiwemo Marais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na wenyeviti wa Baraza la Mapinduzi (wastaafu), Dk. Salmin Amour Juma na Dk. Ali Mohamed Shein, nyakati tofauti katika makazi yao, pamoja na wazee wa CCM kwenye mikutano yao ya mabaraza, Pemba na Zanzibar.

“Asanteni. Waambie pia nawasalimia. Simamieni Chama…chama kijengwe, kisimamiwe kupata ushindi mzuri,” amesema Dk. Salmin Amour, baada ya kufikishiwa salaam za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussen Ali Mwinyi, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,” amesema

Kwa upande wa Dk. Shein, amesisitiza umuhimu wa CCM kuendelea kusimamia misingi ya kuanzishwa kwake.

“CCM ni chama makini sana. Kina misingi na taratibu zake. Na jambo zuri ni kwamba Katibu Mkuu ndiye msimamizi. Nakujua, tumekuwa wote Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa muda mrefu, sina shaka nawe kuyasimamia haya. Tukipindisha taratibu tutaanza kwenda kombo, jingine ni suala la usiri wa vikao, lazima vikao viwe na siri,” amesema Dk. Shein.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here