Home KITAIFA KAMPUNI YA GESI ORYX YAMPA UBALOZI SHILOLE

KAMPUNI YA GESI ORYX YAMPA UBALOZI SHILOLE

Google search engine
Msanii wa muziki wa kizazi kipya na Mama Lishe Zuwena Mohammed maarufu Shilole akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya kutangazwa na Kampuni ya Oryx Gas Tanzania kuwa Balozi wa Kampuni hiyo kwa ajili ya kuhamasisha nishati safi ya kupikia nchini
Mama Lishe na Msanii Zuwena Mohammed ‘Shilole’ akielezea umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia baada ya Kampuni ya Oryx Gas Tanzania kumtangaza kuwa Balozi wa Kampuni hiyo kwa ajili ya kuhamasisha nishati safi ya kupikia kwa Watanzania

Na MWANDISHI WETU

-DAR ES SALAAM

KAMPUNI ya Gesi ya Oryx  imemtangaza Mama Lishe Zuwena Mohamed maarufu Shilole (Shishifood) kuwa balozi wao katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi kupikia kupitia mitungi ya gesi nchini.

Lengo la Oryx kumpa Ubalozi Shilole unalenga kuunga mkono juhudi za Rais Dk. Samia Suluhu ambaye ameweka malengo kuwa ifikapo mwaka 2032 asilimia 80 ya Watanzania iwe inatuminia nishati safi ya kupikia.

Akizungumza wakati wa tukio hilo lililofanyika Julai 4 kwenye Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, Meneja Mauzo na Masoko wa Oryx Gas Shaban Fundi amesema wameamua kumchagua Shilole kwasababu ni miongoni mwa wadau wanaohamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema kupitia kwa Shilole wanaamini kuna wengine ambao walikuwa nyuma kwenye matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kuendelea kutumia gesi za Oryx kupikia.

“Tunafamu Shilole amekuwa mjasiriamali maarufu machi, anamiliki migahawa ya Shishifood katika miji ya Dar es Salaam na Dodoma, amekuwa mama Lishe wa kisasa na muumini  mzuri wa kutunza mazingira,hivyo Oryx tunaona fahari kumtangaza Shilole kuwa balozi wetu katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ili kwa pamoja kufikia malengo ya Rais Samia ya kuhamasisha nishati safi ya kupikia nchini,” amesema

Kwa upande wake Shilole ambaye pia ni Msanii maarufu nchini,amesema yupo tayari kushirikiana na wadau wengine kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema Kampuni ya Oryx imekuwa ikiweka jitihada kubwa kuhamasisha matumizi nihati safi ya kupikia kwa Mama lishe na baba lishe nchini, hivyo ameona kuna umuhimu mkubwa wa kutoa ushirikiano.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here