Home KITAIFA WAZIRI BASHE AZUNGUMZIA UJENZI WA VIHENGE, AIPONGEZA TBA

WAZIRI BASHE AZUNGUMZIA UJENZI WA VIHENGE, AIPONGEZA TBA

Google search engine
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe akizungumza na watendaji wa Wakala wa Chakula wa Taifa (NFRA) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Raymond Mndolwa
Vihenge vipya vilivyojengwa mkoani Rukwa

Na MWANDISHI WETU

-RUKWA

WAZIRI wa Kilimo, Hussein Bashe amesema sababu ya nusu ya mradi wa vihenge mkoani Rukwa kuchelewa kukamilika akitaja mgogoro uliotokea na mkandarasi, japokuwa tayari wametatua changamoto hizo.

Waziri Bashe amesema hayo Julai 16, 2024 wakati akizungumzia ujenzi wa vihenge hivyo ambavyo vimezinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

“TBA (Wakala wa Majengo Tanzania) wamesimamia mradi huu tangu 2019/2020 na wamekamilisha nusu ya mradi lakini, nusu haijakamilika kwasababu kuliingia mgogoro kidogo na mkandarasi…tumewaagiza walimalize hilo ili tumalizie vihenge vingine.

“Rais ametoa maelekezo ya kuongeza vihenge na tumeshakubaliana na Mkurugenzi Mtendaji wa NFRA (Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula) kwa ajili ya kuongeza vingine,”amesema Waziri Bashe.

Waziri Bashe amepongeza usimamizi uliofanywa na TBA hadi kukamilika kwa mradi huo awamu ya kwanza kwa asilimia 100.

Google search engine

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here